Inaonekana mzimu wa madiwani waliounga mkono juhudi za Rais John Magufuli unaanza kukitesa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Hai na mkoa wa Kilimanjaro. Kikundi cha watu kama 200 kilipewa fedha ili tarehe 30 Julai 2020 kiandamane kwenda ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Bwana Lengai Ole Sabaya kupinga matokeo kura ya maoni kata ya KIA. Tumeelezwa kuwa katika ...

Rais John Magufuli na mwenzake wa Uganda, Yoweri Museveni wamekubaliana kurejesha kwenye Ikulu zao mchakato wa kutandaza bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki. Bomba hilo linaloanzia Hoima, Uganda na kuishia Chongoleani, Tanga nchini Tanzania, limekwama baada ya kuwepo kwa “vizingiti” ndani ya serikali zao na  hata wawekezaji katika mradi huo. Wawekezaji katika mradi huo mkubwa wa kusafirisha mafuta, ni Total, Tullow ...

Mgombea wa CCM aliyeongoza kura za maoni Jimbo la Moshi Mjini, Ibrahim Shayo amekutana kwa siri na masheikh watatu wa BAKWATA akisaka kupata ushawishi wao ili aweze kupitishwa na vikao vya juu vya chama hicho. Katika kikao chao cha siri kilichofanyika  Julai 29, 2020 taarifa zetu zinabainisha kuwa wamekubaliana kwamba kila linalowezekana lifanyike ili jina la mgombea huyo lirejeshwe na ...

PrecisionAir, Tanzania’s private commercial airline, has asked its staff, including pilots, to choose; either stay or leave.  In a June 27 internal memo, the airline’s management told staff who choose to leave to table a resignation letter and those opting to stay, write a commitment letter accepting salary cut.  The cut is said to stand down to a quarter of ...

Kampuni ya Mwananchi Communications Limited, wachapaji wa magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti, imewataka waandishi wake wengi kuacha kazi au kubaki kuwa wachangiaji (correspondents). Wachangiaji katika Vyombo vya Habari hapa nchini hulipwa kwa habari (story) zinazochapishwa, wakati mwandishi hulipwa mshahara kwa mwezi. Hatua hii inatajwa kuwa ni njia ya kupunguza matumizi kutokana na kukumbwa na mdororo wa uchumi na ...

Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2020 wa kupata rais, wabunge na madiwani, utalazimika kutumia kiasi cha fedha kutoka Akiba ya Fedha za Kigeni (GOR). ​Hatua hii inatokana na Serikali kukwama kupata fedha za kutosha kugharamia uchaguzi huo kutoka kwa nchi wahisani kama ilivyozoeleka kwa miaka mingi. Sehemu kubwa ya fedha za Uchaguzi husimamiwa na Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) na kwa ...

Pamoja na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Rais John Magufuli na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Bashiru Ally kuonya viongozi wa chama ambao ni wasimamizi kutokuwa na wagombea wao mifukoni, hali imekuwa tofauti majimbo matatu ya mkoa wa Kilimanjaro. Haya ndo tuliyobaini kwa ufupi na uongozi wa CCM Taifa unaweza kutumia vyanzo vyake kubaini undani wa uchunguzi wetu: Jimbo ...

Ofisi ya mawakili wa kimataifa, Amsterdam and Partners inayoshika mikoba ya kumwakilisha Tundu Lissu kisheria, imesema inajiandaa kutangaza matokeo ya uchunguzi juu ya kushambuliwa kwa mteja wake. Taarifa zinaeleza kuwa mawakili hao wanajiandaa kutangaza matokeo ya uchunguzi wao muda wowote kuanzia sasa baada ya kile kinachoelezwa “Serikali kushindwa majukumu yake.” Inaelezwa kuwa mawakili hao mara baada ya kupewa kandarasi ya kumsimamia ...

YAMEIBUKA madai mazito ya uwepo wa matukio ya rushwa kwenye kinyang’anyiro cha kumsaka mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwenye nafasi ya ubunge jimbo la Arusha Mjini. Mbinu alizotumia Makonda huko Kigamboni zinafanana. Aidha msimamizi wa Uchaguzi huo adaiwa kuonyesha upendeleo wa wazi kwa baadhi ya wagombea kwa kuzuia mmoja wa wagombea asiulizwe maswali licha ...

Mkakati wa timu ya Makonda kuhakikisha zinapatikana kura nyingi za maoni kutoka kwa wajumbe wa mkutano mkuu Jimbo la Kigamboni uligubikwa kwa rushwa, imebainika. Rushwa hiyo iliyotembezwa waziwazi kwa wajumbe wa mkutano huo uliomalizika leo, imedhihiri baada ya wapambe wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuanza kuwatukana na kuwatisha baadhi ya wajumbe hao. Waliokula pesa ...